Sunday, June 30, 2013

Rais wa Marekani, Barack Obama anatua nchini kwa ziara ya siku mbili ikiwa ni hatua yake ya mwisho ya ziara yake barani Afrika.



Rais wa Marekani, Barack Obama anatua nchini kwa ziara ya siku mbili ikiwa ni hatua yake ya mwisho ya ziara yake barani Afrika.
Dar es Salaam. Yametimia! Baada ya siku kadhaa za kusubiri kwa hamu, vitabu vya historia ya Tanzania vinaongezewa kumbukumbu wakati Rais wa Marekani, Barack Obama atakapowasili nchini leo mchana kwa ziara ya siku mbili. Ndege ya Air Force One itakayombeba  Obama na msafara wake itakanyaga ardhi ya Tanzania saa 8.40 mchana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambako atapokelewa na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete.
 Obama ambaye anafuatana na mkewe Michelle na binti zake, Malia na Sasha, anatua Tanzania ikiwa ni sehemu yake ya mwisho ya ziara yake barani Afrika.
Anawasili Tanzania akitokea Afrika Kusini ambako alikwenda Ijumaa baada ya ziara yake ya Senegal.
Historia imetimia
Imepita miaka 50, tangu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alipotembelea Marekani, Julai 13, 1963 na kukutana rais wa nchi hiyo wakati huo, John F Kennedy na ziara hiyo inaaminika kuanzisha urafiki wa viongozi hao ambao umedumu hadi sasa. 
Ujio wa Rais Obama una maana na faida kubwa kwa Tanzania katika maeneo ukiangalia kihistoria, kisiasa, kidiplomasia na kiuchumi pia.
Ziara ya  Obama ni heshima kubwa kwa Tanzania na itaingia katika vitabu vya kihistoria kwani ana rekodi ya kuwa mtu mweusi wa kwanza kuchaguliwa kuongoza taifa la Marekani. Kuchaguliwa kwake (Obama), ambaye baba yake mzazi alikuwa na asili ya Kenya kuliashiria nuru mpya kwa siasa za Marekani kwani watu weusi wa taifa hilo kwa miaka mingi walikuwa wakipigania haki za kufaidika na fursa za kiuchumi na kisiasa katika taifa la Marekani.
Tanzania, kwa miaka mingi ilikuwa inaunga mkono harakati za watu weusi na ndiyo maana iliikuwa karibu na viongozi wa harakati za kupigania haki za watu weusi.
Mwalimu Julius Nyerere alikuwa karibu na Martin Luther King na mkewe Correta , ambao waliongoza harakati za mtu mweusi kujikomboa.Pia, viongozi wengine wa harakati hizo za mtu mweusi kutambuliwa kule Marekani, Jesse Jackson, Andrew Young na Malcolm X waliitembelea Tanzania mara nyingi.    Obama alipochaguliwa kushika nafasi hiyo mwaka 2008 alifurahiwa na wapenda amani kote duniani na hasa Waafrika kwani walimhesabu kuwa ni sehemu yao.
Kuja kwake leo ni heshima kubwa kwani Tanzania inakuwa nchi ya nne  Afrika kutembelewa na Obama baada ya Ghana mwaka 2009 na ziara yake ya hivi karibuni ya nchi za Senegal na Afrika Kusini.

Ukizingatia kuwa  Obama  ana miaka mitatu na nusu kabla ya kumaliza kipindi chake cha pili cha uongozi wake huenda ziara hii ndiyo ikawa ya mwisho kwake barani Afrika akiwa na wadhifa wa rais.

Wednesday, June 26, 2013

UJIO WA RAIS OBAMA NCHINI TANZANIA


Rais wa Marekani Bw. Baraka Obama na Mkewe wanatarajia kufanya ziara ya nchi tatu barani Afrika itakayojumuisha nchi za Senegal, Afrika ya Kusini na Tanzania, Kuanzia tarehe 26 Juni hadi tarehe 3 Julai. 
Katika ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, uwekezaji na biashara, uimarishaji wa taasisi za kidemokrasia na uwekezaji katika kizazi kipya cha viongozi wa Kiafrika.
Rais atakutana na viongozi mbalimbali wa kiserikali, sekta binafsi na jumuiya huru ya kiraia ikiwemo vijana ili kujadili ubia wetu wa kimkakati katika ushirikano wetu rasmi na masuala mengine ya kimataifa.
 
Ziara hii itadhihirisha dhamira ya dhati ya Rais ya kupanua na kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na watu wa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika kuimarisha amani na ustawi katika kanda hii na duniani kote kwa ujumla.


Saturday, June 15, 2013

Upepo mkali waezua madarasa matano Rorya


Rorya. Upepo mkali umeezua vyumba vitano vya madarasa na ofisi moja ya walimu katika Shule ya Msingi Kogaja,Kata ya Ikoma katika Wilaya ya Rorya Mara.
Akitoa taarifa kwa Mbunge wa Jimbo la Rorya, Lameck Airo wakati alipotembelea na kuangalia maafa hayo,Afisa Mtendaji wa kijiji hicho,Lucas Ombonya alisema hata hivyo katika maafa hayo hakuna mtu yeyote ambaye alijeruhiwa kwa kuwa shule hiyo ilikuwa imefungwa kufuatia likizo ya mwezi wa sita.
Hata hivyo,Ombonya alisema tathmini ambayo ilifanywa na kamati ya maafa ya kijiji hicho ilibaini kuwa zinahitajika Sh9.2 milioni ili kurejesha majengo hayo katika hali yake ya kawaida.
Kwa upande wake,mbunge wa jimbo hilo alisema watahakikisha wanatatua tatizo hilo la maafa kwa shule hiyo na kulaani vitendo vya baadhi ya viongozi kuhamasisha ubaguzi wa itikadi za kisiasa kwa kile alichodai kuwa ni kuzorotesha maendeleo ya kijamii.
Mbunge huyo alitoa kiasi cha Sh3milioni kama mchango wake binafsi kwa ajili ya kuboresha shule hiyo,huku akiwataka na wengine walioguswa na maafa hayo kuchangia.
Naye Mwenyekiti wa CCM Rorya,Samwel Kiboye,kabla ya kutoa mchango wake wa Sh1milioni aliwataka wananchi kuepuka vurugu wakati wa kutoa maoni yao ya kuchangia rasimu ya katiba ili kuwezesha kupata maoni ambayo yatawezesha taifa kupata katiba nzuri.
Katika ziara hiyo ya kukagua maafa hayo,mbunge huyo ameitisha harambee ya papo kwa papo ambapo kiasi cha Sh9milioni kilichokuwa kinahitajika kilipatikana,huku Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rorya, Chaeles Ochere,akichangia Sh1.2 milioni,Halmashauri Sh1.5milioni, huku wananchi wa kijiji hichona diwani wao wakichangia Sh2milioni.

Afa kwa kunywa komoni

MWANAKIJIJI wa Matandalani, Ngusa Solea (32) amefariki dunia baada ya kunywa pombe aina ya komoni inayosadikiwa kuwa na sumu
.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema kifo hicho kilitokea juzi saa tatu asubuhi kwenye kijiji hicho kilichopo kwenye Tarafa ya Nsimbo.

Kwa mujibu wa kamanda huyo, mwili wa marehemu ulikutwa nje ya nyumba inayojengwa jirani na nyumba ya Anisety Matongo ukitokwa damu puani.

“Inaelezwa kwamba marehemu alikuwa akinywa pombe hiyo nyumbani kwa Matongo na haikufahamika aliondoka saa ngapi.
“Chanzo cha kifo hicho kinadhaniwa  kuwa ni pombe yenye sumu,” alisema kamanda huyo na kuongeza hakuna aliyekamatwa kuhusiana na kifo hicho. 

HASSAN HAJI HAMISI

                       HASSAN .HAJI. HAMISI

EMAIL:            hassanhamis60@yahoo.com

CONTACTS:   +255-766 392 186
                         +255-714 797 610
                         +255-687 371 388
                             Arusha.Tz



more Info: http//hassanhamisi.blogspot.com

Tuesday, June 11, 2013

ziara ya obama tanzania

Marekani yataja sababu nne za Obama kuja Tz





. Marekani imetaja sababu nne ambazo zimemfanya Rais Barrack Obama kuijumuisha Tanzania katika ziara yake ya bara la Afrika.
Rais Obama amepanga kulitembelea bara la Afrika kuanzia Juni 26 hadi Julai 3, mwaka huu na atazitembelea pia Senegal na Afrika Kusini.
Kiongozi huyo wa Marekani ambaye baba yake mzazi ni mzaliwa wa Kenya, anatarajiwa kuwasili nchini Julai Mosi kwa ziara ya siku tatu. Atakuwa Rais wa tatu wa Marekani kuitembelea Tanzania baada ya Bill Clinton mwaka 2000 na George Bush mwaka 2008.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Balozi wa Marekani, Alfonso Lenhardt alisema sababu ya kwanza ya Obama kuja Tanzania ni kutokana na kuwa mfano wa utawala bora, demokrasia na ushirikishaji wa watu wake wakati wa kufanya uamuzi unaogusa maisha yao ya kila siku.
Alisema kuwa Tanzania ni nchi ya mfano linapokuja suala la uongozi bora na ndiyo maana imekuwa na amani na utulivu kwa muda mrefu ikilinganishwa na nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.
“Nchi nyingi za Afrika zinazoizunguka Tanzania zimekuwa na matatizo ya vita vya wenyewe na hata ukosefu wa utawala bora,” alisema Balozi Lenhardt ingawa alidokeza kuwa katika siku za karibuni imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali kutokana na matukio ya uvunjifu wa amani.
Balozi Lenhardt alisema sababu nyingine inayomfanya Rais Obama kuja Tanzania ni kutokana na jitihada za Serikali ya Marekani kutengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji na kasi ya ukuaji wa uchumi.
“Rais Obama anakuja kuunga mkono juhudi za Watanzania katika kutengeneza mazuri ya uwekezaji lakini bila kusahau kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania imeivutia Serikali ya Marekani,” alisema.
Balozi Lenhardt alitaja sababu nyingine inayomleta Rais Obama kuwa ni kuisaidia Tanzania kuendeleza fursa mbalimbali za kujiletea maendeleo.
Alisema uendelezaji huo wa fursa una lengo la kuisaidia Serikali ya Tanzania kukabiliana na tatizo la umaskini.
Alisema Marekani ni moja ya nchi zinazoongoza kwa kutoa fedha nyingi za misaada na akisema kwa mfano, mwaka 2012 pekee ilitoa Dola 750 milioni.
Aidha, alisema nchi yake imekuwa ikitoa misaada mingi kupitia Shirika la Millenium Challenge (MCC), ambayo imejikita zaidi katika kusaidia sekta za umeme, maji na miundombinu.