Ngwair alifariki wiki iliyopita nchini Afrika Kusini alikokwenda kwa shughuli
za muziki na mwili wake kuletwa jana mchana, Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere
Dar es Salaam.
Simanzi ilitanda eneo zima la uwanja walikojazama mashabiki wa sanaa ya
muziki, wengi wao wakiwa vijana wakati jeneza la Ngweair likitolewa sehemu ya
ndani ya uwanja na kuletwa nje.
Vilio pia vilitawala kutoka kwa ndugu wa marehemu na watu wengine
walioshindwa kuvumilia baada ya kushuhudia jeneza hilo likitolewa nje tayari kwa
safari ya kupelekwa Hospitali ya Taifa, Muhimbili.
Kutokana na wingi wa watu, vijana wa skauti walilazimika kufanya kazi ya
ziada kuunganisha mikono yao ili gari lililobeba mwili wa Mangwair liweze kupita
bila kuzongwa, jambo lililowashinda
nguvu.
nguvu.
Hali ilikuwa tofauti baada ya kundi la vijana kuendelea kuimba wimbo wa
Kamanda, huku wakisukuma gari lililobeba mwili wa Ngwair na kusababisha
msongamano mkubwa wa magari.
Kadri mwili wa msanii huyo ulivyokuwa ukisogea mbele, ndivyo watu hasa vijana
walivyokuwa wakijitokeza kutoka pembezoni mwa barabara na kuungana na wengine
kusukuma gari.
Kazi ya kusukuma gari hiyo iliendelea kwa muda mrefu kupita barabara kuu ya
Pugu kuelekea Muhimbili, ambako mwili wake ungehifadhiwa kabla ya
kuagwa.
Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania, Ado Novemba alisema mwili wa marehemu
utaagwa leo kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni kuanzia saa mbili asubuhi
mpaka saa sita mchana.
Baada ya hapo, marehemu atasafirishwa kwenda Morogoro kwa ajili ya mazishi
yatakayofanyika kwenye makaburi ya Kihonda.
No comments:
Post a Comment