Rorya. Upepo mkali umeezua vyumba vitano vya madarasa na ofisi moja ya walimu
katika Shule ya Msingi Kogaja,Kata ya Ikoma katika Wilaya ya Rorya
Mara.
Akitoa taarifa kwa Mbunge wa Jimbo la Rorya, Lameck Airo wakati alipotembelea
na kuangalia maafa hayo,Afisa Mtendaji wa kijiji hicho,Lucas Ombonya alisema
hata hivyo katika maafa hayo hakuna mtu yeyote ambaye alijeruhiwa kwa kuwa shule
hiyo ilikuwa imefungwa kufuatia likizo ya mwezi wa sita.
Hata hivyo,Ombonya alisema tathmini ambayo ilifanywa na kamati ya maafa ya
kijiji hicho ilibaini kuwa zinahitajika Sh9.2 milioni ili kurejesha majengo hayo
katika hali yake ya kawaida.
Kwa upande wake,mbunge wa jimbo hilo alisema watahakikisha wanatatua tatizo
hilo la maafa kwa shule hiyo na kulaani vitendo vya baadhi ya viongozi
kuhamasisha ubaguzi wa itikadi za kisiasa kwa kile alichodai kuwa ni kuzorotesha
maendeleo ya kijamii.
Mbunge huyo alitoa kiasi cha Sh3milioni kama mchango wake binafsi kwa ajili
ya kuboresha shule hiyo,huku akiwataka na wengine walioguswa na maafa hayo
kuchangia.
Naye Mwenyekiti wa CCM Rorya,Samwel Kiboye,kabla ya kutoa mchango wake wa
Sh1milioni aliwataka wananchi kuepuka vurugu wakati wa kutoa maoni yao ya
kuchangia rasimu ya katiba ili kuwezesha kupata maoni ambayo yatawezesha taifa
kupata katiba nzuri.
Katika ziara hiyo ya kukagua maafa hayo,mbunge huyo ameitisha harambee ya
papo kwa papo ambapo kiasi cha Sh9milioni kilichokuwa kinahitajika
kilipatikana,huku Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rorya, Chaeles Ochere,akichangia
Sh1.2 milioni,Halmashauri Sh1.5milioni, huku wananchi wa kijiji hichona diwani
wao wakichangia Sh2milioni.
No comments:
Post a Comment