Sunday, June 30, 2013

Rais wa Marekani, Barack Obama anatua nchini kwa ziara ya siku mbili ikiwa ni hatua yake ya mwisho ya ziara yake barani Afrika.



Rais wa Marekani, Barack Obama anatua nchini kwa ziara ya siku mbili ikiwa ni hatua yake ya mwisho ya ziara yake barani Afrika.
Dar es Salaam. Yametimia! Baada ya siku kadhaa za kusubiri kwa hamu, vitabu vya historia ya Tanzania vinaongezewa kumbukumbu wakati Rais wa Marekani, Barack Obama atakapowasili nchini leo mchana kwa ziara ya siku mbili. Ndege ya Air Force One itakayombeba  Obama na msafara wake itakanyaga ardhi ya Tanzania saa 8.40 mchana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambako atapokelewa na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete.
 Obama ambaye anafuatana na mkewe Michelle na binti zake, Malia na Sasha, anatua Tanzania ikiwa ni sehemu yake ya mwisho ya ziara yake barani Afrika.
Anawasili Tanzania akitokea Afrika Kusini ambako alikwenda Ijumaa baada ya ziara yake ya Senegal.
Historia imetimia
Imepita miaka 50, tangu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alipotembelea Marekani, Julai 13, 1963 na kukutana rais wa nchi hiyo wakati huo, John F Kennedy na ziara hiyo inaaminika kuanzisha urafiki wa viongozi hao ambao umedumu hadi sasa. 
Ujio wa Rais Obama una maana na faida kubwa kwa Tanzania katika maeneo ukiangalia kihistoria, kisiasa, kidiplomasia na kiuchumi pia.
Ziara ya  Obama ni heshima kubwa kwa Tanzania na itaingia katika vitabu vya kihistoria kwani ana rekodi ya kuwa mtu mweusi wa kwanza kuchaguliwa kuongoza taifa la Marekani. Kuchaguliwa kwake (Obama), ambaye baba yake mzazi alikuwa na asili ya Kenya kuliashiria nuru mpya kwa siasa za Marekani kwani watu weusi wa taifa hilo kwa miaka mingi walikuwa wakipigania haki za kufaidika na fursa za kiuchumi na kisiasa katika taifa la Marekani.
Tanzania, kwa miaka mingi ilikuwa inaunga mkono harakati za watu weusi na ndiyo maana iliikuwa karibu na viongozi wa harakati za kupigania haki za watu weusi.
Mwalimu Julius Nyerere alikuwa karibu na Martin Luther King na mkewe Correta , ambao waliongoza harakati za mtu mweusi kujikomboa.Pia, viongozi wengine wa harakati hizo za mtu mweusi kutambuliwa kule Marekani, Jesse Jackson, Andrew Young na Malcolm X waliitembelea Tanzania mara nyingi.    Obama alipochaguliwa kushika nafasi hiyo mwaka 2008 alifurahiwa na wapenda amani kote duniani na hasa Waafrika kwani walimhesabu kuwa ni sehemu yao.
Kuja kwake leo ni heshima kubwa kwani Tanzania inakuwa nchi ya nne  Afrika kutembelewa na Obama baada ya Ghana mwaka 2009 na ziara yake ya hivi karibuni ya nchi za Senegal na Afrika Kusini.

Ukizingatia kuwa  Obama  ana miaka mitatu na nusu kabla ya kumaliza kipindi chake cha pili cha uongozi wake huenda ziara hii ndiyo ikawa ya mwisho kwake barani Afrika akiwa na wadhifa wa rais.

Wednesday, June 26, 2013

UJIO WA RAIS OBAMA NCHINI TANZANIA


Rais wa Marekani Bw. Baraka Obama na Mkewe wanatarajia kufanya ziara ya nchi tatu barani Afrika itakayojumuisha nchi za Senegal, Afrika ya Kusini na Tanzania, Kuanzia tarehe 26 Juni hadi tarehe 3 Julai. 
Katika ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, uwekezaji na biashara, uimarishaji wa taasisi za kidemokrasia na uwekezaji katika kizazi kipya cha viongozi wa Kiafrika.
Rais atakutana na viongozi mbalimbali wa kiserikali, sekta binafsi na jumuiya huru ya kiraia ikiwemo vijana ili kujadili ubia wetu wa kimkakati katika ushirikano wetu rasmi na masuala mengine ya kimataifa.
 
Ziara hii itadhihirisha dhamira ya dhati ya Rais ya kupanua na kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na watu wa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika kuimarisha amani na ustawi katika kanda hii na duniani kote kwa ujumla.


Saturday, June 15, 2013

Upepo mkali waezua madarasa matano Rorya


Rorya. Upepo mkali umeezua vyumba vitano vya madarasa na ofisi moja ya walimu katika Shule ya Msingi Kogaja,Kata ya Ikoma katika Wilaya ya Rorya Mara.
Akitoa taarifa kwa Mbunge wa Jimbo la Rorya, Lameck Airo wakati alipotembelea na kuangalia maafa hayo,Afisa Mtendaji wa kijiji hicho,Lucas Ombonya alisema hata hivyo katika maafa hayo hakuna mtu yeyote ambaye alijeruhiwa kwa kuwa shule hiyo ilikuwa imefungwa kufuatia likizo ya mwezi wa sita.
Hata hivyo,Ombonya alisema tathmini ambayo ilifanywa na kamati ya maafa ya kijiji hicho ilibaini kuwa zinahitajika Sh9.2 milioni ili kurejesha majengo hayo katika hali yake ya kawaida.
Kwa upande wake,mbunge wa jimbo hilo alisema watahakikisha wanatatua tatizo hilo la maafa kwa shule hiyo na kulaani vitendo vya baadhi ya viongozi kuhamasisha ubaguzi wa itikadi za kisiasa kwa kile alichodai kuwa ni kuzorotesha maendeleo ya kijamii.
Mbunge huyo alitoa kiasi cha Sh3milioni kama mchango wake binafsi kwa ajili ya kuboresha shule hiyo,huku akiwataka na wengine walioguswa na maafa hayo kuchangia.
Naye Mwenyekiti wa CCM Rorya,Samwel Kiboye,kabla ya kutoa mchango wake wa Sh1milioni aliwataka wananchi kuepuka vurugu wakati wa kutoa maoni yao ya kuchangia rasimu ya katiba ili kuwezesha kupata maoni ambayo yatawezesha taifa kupata katiba nzuri.
Katika ziara hiyo ya kukagua maafa hayo,mbunge huyo ameitisha harambee ya papo kwa papo ambapo kiasi cha Sh9milioni kilichokuwa kinahitajika kilipatikana,huku Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rorya, Chaeles Ochere,akichangia Sh1.2 milioni,Halmashauri Sh1.5milioni, huku wananchi wa kijiji hichona diwani wao wakichangia Sh2milioni.

Afa kwa kunywa komoni

MWANAKIJIJI wa Matandalani, Ngusa Solea (32) amefariki dunia baada ya kunywa pombe aina ya komoni inayosadikiwa kuwa na sumu
.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema kifo hicho kilitokea juzi saa tatu asubuhi kwenye kijiji hicho kilichopo kwenye Tarafa ya Nsimbo.

Kwa mujibu wa kamanda huyo, mwili wa marehemu ulikutwa nje ya nyumba inayojengwa jirani na nyumba ya Anisety Matongo ukitokwa damu puani.

“Inaelezwa kwamba marehemu alikuwa akinywa pombe hiyo nyumbani kwa Matongo na haikufahamika aliondoka saa ngapi.
“Chanzo cha kifo hicho kinadhaniwa  kuwa ni pombe yenye sumu,” alisema kamanda huyo na kuongeza hakuna aliyekamatwa kuhusiana na kifo hicho. 

HASSAN HAJI HAMISI

                       HASSAN .HAJI. HAMISI

EMAIL:            hassanhamis60@yahoo.com

CONTACTS:   +255-766 392 186
                         +255-714 797 610
                         +255-687 371 388
                             Arusha.Tz



more Info: http//hassanhamisi.blogspot.com

Tuesday, June 11, 2013

ziara ya obama tanzania

Marekani yataja sababu nne za Obama kuja Tz





. Marekani imetaja sababu nne ambazo zimemfanya Rais Barrack Obama kuijumuisha Tanzania katika ziara yake ya bara la Afrika.
Rais Obama amepanga kulitembelea bara la Afrika kuanzia Juni 26 hadi Julai 3, mwaka huu na atazitembelea pia Senegal na Afrika Kusini.
Kiongozi huyo wa Marekani ambaye baba yake mzazi ni mzaliwa wa Kenya, anatarajiwa kuwasili nchini Julai Mosi kwa ziara ya siku tatu. Atakuwa Rais wa tatu wa Marekani kuitembelea Tanzania baada ya Bill Clinton mwaka 2000 na George Bush mwaka 2008.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Balozi wa Marekani, Alfonso Lenhardt alisema sababu ya kwanza ya Obama kuja Tanzania ni kutokana na kuwa mfano wa utawala bora, demokrasia na ushirikishaji wa watu wake wakati wa kufanya uamuzi unaogusa maisha yao ya kila siku.
Alisema kuwa Tanzania ni nchi ya mfano linapokuja suala la uongozi bora na ndiyo maana imekuwa na amani na utulivu kwa muda mrefu ikilinganishwa na nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.
“Nchi nyingi za Afrika zinazoizunguka Tanzania zimekuwa na matatizo ya vita vya wenyewe na hata ukosefu wa utawala bora,” alisema Balozi Lenhardt ingawa alidokeza kuwa katika siku za karibuni imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali kutokana na matukio ya uvunjifu wa amani.
Balozi Lenhardt alisema sababu nyingine inayomfanya Rais Obama kuja Tanzania ni kutokana na jitihada za Serikali ya Marekani kutengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji na kasi ya ukuaji wa uchumi.
“Rais Obama anakuja kuunga mkono juhudi za Watanzania katika kutengeneza mazuri ya uwekezaji lakini bila kusahau kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania imeivutia Serikali ya Marekani,” alisema.
Balozi Lenhardt alitaja sababu nyingine inayomleta Rais Obama kuwa ni kuisaidia Tanzania kuendeleza fursa mbalimbali za kujiletea maendeleo.
Alisema uendelezaji huo wa fursa una lengo la kuisaidia Serikali ya Tanzania kukabiliana na tatizo la umaskini.
Alisema Marekani ni moja ya nchi zinazoongoza kwa kutoa fedha nyingi za misaada na akisema kwa mfano, mwaka 2012 pekee ilitoa Dola 750 milioni.
Aidha, alisema nchi yake imekuwa ikitoa misaada mingi kupitia Shirika la Millenium Challenge (MCC), ambayo imejikita zaidi katika kusaidia sekta za umeme, maji na miundombinu.


Thursday, June 6, 2013

‘Chamber Squad’

BAADA ya ‘sintofahamu’ na taharuki iliyowakumba wanamuziki hasa kundi la Chamber Squad baada ya kifo cha msanii mwenzao, Albert Mangwea ‘Ngwair,’ swahiba wake, Mez B, anatoa wasifu wa ‘Ngwair’ kama ifuatavyo:
“Tunasema asante Mungu kupata nafasi hii kusema machache kuhusu ndugu yetu Albert Mangwea ‘Ngwair’ ‘Cow Obama.’
Sisi kama Chamber Squad, tungependa kumzungumzia zaidi kama ‘Ngwair’ na si kama Albert, maana tayari ameshazungumziwa katika risala nyingi,” hivi ndivyo anavyoanza kusema Mez B.
Anasema: “Kwa kifupi, Ngwair tulikutana kwa mara ya kwanza Shule ya Sekondari ya wavulana Mazengo iliyopo mkoani Dodoma mwaka 1997 wakati huo akiwa kidato cha kwanza.
“Kipindi hicho tulikutana na kaka zetu ambao ni Augustino Makale a.k.a Tino na Athumani Kabongo a.k.a. Dark Master. Hawa ndio waasisi wa Chamber Squad pamoja na kaka zetu, Alkapaono, G2 The Bye na Mussa Gama.”
Maana halisi ya Chamber Squad
“Ni vyumba vya kusomea ambavyo kaka zetu hawa walikuwa wanakesha humo wakijisomea usiku kucha na wanapochoka, ndipo redio zinawashwa na ‘Freestyle’ zinaanza kupooza.
“Tulihamasika na ‘style’ yao , ndipo sisi pia tukaunda kundi dogo lililojulikana kwa jina la ‘Chamber Flavor Guys (C.F.G) lililoundwa na mimi ‘QG’, ambaye kwa sasa nafahamika kama Mez B, Mangwea na Malo Star, ambaye kwa sasa hafanyi kazi ya muziki.”
Asili ya jina la Ngwair
Mez B anasema jina la ‘Ngwair’ halikutokea hewani tu, lilitokana na jina lake halisi la Mangwea, ambapo wakati wanasoma Mazengo, walikuwa na kawaida ya kucheza mpira wa kikapu hadi usiku wa manane.
“Hiyo ikatufanya tumuite ‘Man In The Air’ kutokana na ukali wake wa kupiga ‘free throws’ ndipo jina la Mangwair lilipozaliwa mpaka kuwa ‘Ngwair’,” anasema Mez B.
“Mwaka uliofuata (1998), tulitoa albamu yetu ya kwanza iliyofahamika kwa jina la ‘Heshima kwa Wote’, tulirekodi chini ya mtayarishaji Xpela katika Studio ya Tushikamane iliyopo mkoani Morogoro ambayo ilisambazwa na Wananchi Store.
Baada ya kuhitimu elimu yetu ya sekondari, tuliamua kama ‘Chamber Flavor Guys’ kuwa chamber rasmi na kujiunga na Dark Master, hapo pia akaingia Noorah na Tony, ambapo maskani yetu yalikuwa Kijitonyama kwenye makazi ya Tony.
“ Tuliweza kutengeneza nyimbo kama ‘Ahadi za Boss’, ‘Party East Zoo’ na Shega Tuu’, ndipo mwenzetu alipoweza kupata nafasi ya kurekodi ‘Gheto Langu’ ndani ya Studio ya Bongo Records ikiwa chini ya P. Funk ‘Majani.’
“Baada ya hapo, alitoa albamu yake ya kwanza ya ‘a.k.a. Mimi,’ chini ya usimamizi wa DJ Venture ambayo ilisababisha kushinda tuzo mbili za muziki za Kilimanjaro Music Awards ambazo ni albamu bora ya Hip Hop na wimbo bora wa kushirikiana,” anasema.
Huu ndio ukawa mwanzo wa kutoa ‘hit’ baada ya ‘hit’ ya nyimbo nyingi ambazo ni ‘Kama Vipi’ ya Mez B’, ‘Ice Cream’ ya Noorah na nyingine nyingi pamoja na kufanya maonesho kadhaa.
“Rafiki yetu alikuwa mtu mchangamfu na mwenye vituko sana, huwezi kukaa naye bila kucheka. Na uwezo wake wa kukariri nyimbo na uthubutu wa kila jambo vilikuwa ni vitu tofauti sana kulingana na umri wake siku zote za uhai wake,” anasema Mez B.
Ngwair na umeneja wa klabu
“Nakumbuka wakati tuko kidato cha nne, Ngwair alikuwa tayari ni Meneja wa Club ya La Azizi iliyopo Dodoma, tukienda jioni tunakuta mwenzetu ameshika kipaza sauti ‘Mic’ anaimbisha jukwaani na wachezaji ‘dancers’ tukianzia kuelezea vituko tulivyopitia tutatumia hata siku nzima, lakini havitaisha na kuchekesha.
“Tunawashukuru Watanzania kujitokeza kwa wingi, hii inaonesha jinsi gani upendo mlionao kwa ndugu yetu. Mimi Mez B, Dark Master, Noorah na close friends wake Ben Mshua, Thuwein na Pius tunaahidi tutaendeleza alichokiacha njiani, tunaomba mwendelee kutuonesha upendo huu na ushirikiano wenu,” anasema Mez B.
Mangwair aliyefariki dunia Mei 28 nchini Afrika Kusini na kuzikwa Juni 6, nyumbani kwao Kihonda, mkoani Morogoro, kwa hakika ameondoka huku mchango wake kwenye ‘gemu’ na taifa kwa ujumla ukiwa bado unahitajika.
Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya Mangwair. Amina.

Polisi yawatosa askari 12

HATIMAYE Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, limeamua kuwafukuza kazi askari wake 12 wanaotumiwa kujihusisha na biashara za magendo na kuwalinda wafanyabiashara wanaokwepa kodi.
Awali kabla ya hatua hiyo kufikiwa askari 16 walikuwa wakishikiliwa katika kituo cha kati na uchunguzi uliofanyika dhidi yao wanne walibainika kutohusika na tuhuma hizo.
Tanzania Daima imedokezwa kuwa askari 12 waliofukuzwa kazi wakati wowote kuanzia sasa watafikishwa katika mahakama za kiraia kujibu mashtaka yao.
Habari za uhakika kutoka ndani ya jeshi hilo zinapasha kwamba jana askari wote 16 walikuwa wakishikiliwa katika kituo cha polisi Kati kabla ya kuhamishiwa kituo cha Kijitonyama (Mabatini) walikosomewa hukumu yao.
Askari hao walisomewa hukumu hiyo na Kamanda mpya wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, aliyeripoti kazini mwanzoni mwa wiki hii akitokea mkoani Arusha alikokuwa akishikilia wadhifa wa Mkuu wa Upelelezi Mkoa (RCO).
“Wambura kaingia kwa kishindo, kawasomea hukumu leo asubuhi wale askari waliokuwa mahabusu, wanne wameachiwa huru na wamesema wenzao wamefukuzwa kazi,” kilisema chanzo cha habari.
Tanzania Daima, iliwasiliana kwa njia ya simu na afande Wambura juu ya hukumu yake ya kuwatia kitanzini askari 12 ambapo alisema suala hilo mwenye uwezo wa kulizungumzia ni Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova.
“Hilo ni suala kubwa sana kwangu, ni la kanda, mpigie kamanda wa Kanda Maalum atakupa kila kitu unachohitaji,” alisema Wambura.
Tanzania Daima, lilipowasiliana na Kamanda Kova alihoji gazeti lilivyopata habari hizo kabla hazijafika ofisini kwake.
“Unapataje taarifa hizo kabla hazijafika kwangu wakati mimi nazisubiri? Huyo jamaa anakupaje taarifa kabla ya kufika kwangu? Mwambie aliyekupa hizo taarifa akwambie yote,” alisema.
Hata hivyo Kamanda Kova aliitaka Tanzania Daima impe muda zaidi alishughulikie jambo hilo na likiwa tayari ataliweka wazi kwa umma.
Mwanzoni mwa mwezi uliopita, Tanzania Daima, iliandika habari za polisi na baadhi ya maofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kujihusisha na biashara za magendo na kuwakingia kifua wafanyabiashara wanaokwepa kodi Kamuhanda ahamia Dar
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP, Saidi Mwema, amemhamishia makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda.
Kamuhanda anakumbukwa kwa kusimamia operesheni ya jeshi hilo mkoani Iringa dhidi ya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliokuwa wakifungua tawi la chama hicho katika kijiji cha Nyololo Septemba 2 mwaka jana katika operesheni hiyo mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Chanel Ten, Daudi Mwangosi, aliuawa na bomu lililodaiwa kutoka kwa mmoja wa askari waliokuwa wakimdhibiti mwandishi huyo.
Kutokana na mabadiliko hayo nafasi ya Kamuhanda imechukuliwa na ACP, Ramadhan Mungi (aliyekuwa Makao Makuu ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai).
Katika taarifa ya Jeshi la Polisi kwa vyombo vya habari, mbali na Kamuhanda, makamanda wengine waliohamishwa ni ACP Charles Kenyela (RPC Kinondoni) aliyehamishiwa makao makuu ya upelelezi wa makosa ya jinai.
DCP, Ally Mlege, aliyekuwa Makao Makuu ya Polisi amehamishiwa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na kuwa mkuu wa utawala na rasilimali watu.
ACP Duwani Nyanda aliyekuwa makao makuu ya idara ya upelelezi amehamishiwa mkoani Arusha kuwa mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa uhamisho huo ni wa kawaida kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi.

CHADEMA yajipanga kuikosoa rasimu ya Katiba

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepanga kutoa tamko kuhusu rasimu ya mabadiliko ya Katiba iliyotangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba.
Akizungumza na Tanzania Daima jana Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri wa CHADEMA John Mrema alisema kwa sasa viongozi wa juu na watalaamu wanaisoma na kuichambua.
“Hatuwezi kutoa maoni ya juu juu kuhusu rasimu ya katiba… ni kitu nyeti ambacho kinatakiwa kufanyiwa kazi kwanza ili chama kitakapozungumzwa iwe kwa ajili ya manufaa ya Watanzania wote na si ya mtu mmoja ndiyo maana kazi hii tumeikabidhi kwa wataalam,” alisema Mrema.
Pamoja na mambo mengi wachambuzi hao watapitia mambo yaliyokubaliwa na yaliyoachwa ili kuionyesha tume hiyo kuwa kuna ambayo yana manufaa kwa taifa ingawa wameyaacha.
Katika rasimu hiyo mambo yaliyoachwa ni pamoja na serikali ya majimbo kwa sababu kuwa gharama za kuiendeshea zitaongezeka endapo serikali tatu zitakuwapo pamoja kuweza kufumuka mambo ya udini, malalamiko, dalili za kujitenga, ukabila na ukanda.
Mambo mengine yaliyokataliwa katika serikali ya muungano ni Mahakama ya Kadhi kwa maelezo kwamba nchi washirika zinaweza kulijadili.

.Uingereza yakubali kuwafidia Mau Mau

Uingereza imekubali kuwalipa fidia na kuwaomba msahama walioteswa wakati wa ukoloni wa Muingereza Kenya
Serikali ya Uingereza imetangaza kuwa itawalipa fidia ya dola milioni thelathini manusura wa harakati za ukombozi wa Uhuru wa Kenya Mau Mau.
Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague ametangaza kuwa serikali yake itawalipa wale wote walioteswa na askari wa ukoloni katika miaka ya 1950.
Waliokuwa wanachama wa vuguvugu hilo waliwasilisha kesi mahakamani kwa mateso na dhuluma walizodai kutendewa na uliokuwa utawala wa ukoloni miaka ya 50.Huenda pia Uingereza itatangaza fidia.
Zaidi ya wakenya 5,000, waliteswa baadhi wakinyanyaswa na waliokuwa wakoloni wa Uingereza.
Uingereza ilipigana vita vikali dhidi ya Mau Mau, waliokuwa wanadai ardhi na kuondoka kwa utawala wa kikoloni.
Baadhi ya waliokuwa wanachama wa Mau Mau
Manusura wa vita hivyo wamekuwa wakiidai Uingereza kuwalipa fidia kwa miaka mingi.
BBC ina habari kuwa bwana Hague atawaomba radhi waathiriwa wa vita vya Mau Mau, wakati akitangaza kiwango cha pesa watakazotoa kama fidia kwao.
Serikali ya Uingereza awali ilikuwa imesema kuwa madai yote ya vitedno walivyofanya wakoloni ni juu ya serikali ya Kenya tangu kuipa uhuru mwaka 1963 na kuwa kwa sasa haiwezi kutakiwa kulipa.
Lakini mwaka 2011, mahakama iliamuru kuwa, wanaodai fidia, Paulo Muoka Nzili, Wambuga Wa Nyingi na Jane Muthoni Mara, walikuwa na haki ya kudai fidia kutoka kwa Uingereza .
Mawakili wao wanasema kuwa Nzili alihasiwa , huku Bwana Nyingi akichapwa vibaya wakati Bi Mara akiteswa kimapenzi katika kambi za mateso ambako waliokuwa wanapinga ukoloni walikuwa wakifungwa.
Baada ya uamuzi wa kesi hiyo, ilirejeshwa katika mahakama kuu ili kuamua pesa watakazolipwa na ofisi ya jumuiya ya madola.
Mahakam kuu Uingereza iliamua kuwa walalmishi walipaswa kutendwa haki
Duru zinasema kuwa serikali ilikumbwa na wakati mgumu kupata mashahidi na stakabadhi muhimu kuweza kuelezea ukweli katika kesi hiyo.
Lakini Oktoba mwaka jana, mahakama iliamua kuwa waathiriwa waliowasilisha kesi hiyo mahakamani walikuwa na haki ya kufidiwa kwani walikuwa na kesi nzito dhidi ya serikali ya Uingereza.
Watatu hao walikuwa wamesema kuwa wangekubali wahusika wa kesi kuafikiana nje ya mahakama lakini pia walikuwa wanataka kufuata sheria kwani waliona wangepata haki katika mahakama.....

MJ RADIO







































Watoto wabobea ulevini Ulaya



Mtoto Mlevi
Sasa tatizo la ulevi lawavamia watoto chini ya umri wa miaka 10 chini Uingereza huku wengine wakilazwa hospitalini.
Wataalam wanasema karibu watoto wapatao 380 wamefikishwa hispitalini na kulazwa kutokana na kuchanganyikiwa kulikosababishwa na ulevi.
Kunywa pombe Uzeeni ni hatari kwa akili . mzee huanza kuwa na matatizo ya kusahau sahau na kuonekana mkosa hekima na busara

Nutrition


Nutrition 'must be a global priority', say researchers


Child
      Malnutrition is responsible for 45% of the global deaths of children under the age of five, research published in the Lancet medical journal suggests.
Poor nutrition leads to the deaths of about 3.1 million under-fives annually, it says.
An international team reviewed different causes of malnutrition in pregnancy and childhood.
They say the first 1,000 days of life - from conception to two years - have lasting consequences for health.
Malnutrition - which includes being overweight or obese as well as under-nourished - also has an economic impact.
According to a recent United Nations report, malnutrition is estimated to cost the world $3.5tn (£2.3tn) - or $500 for every person - in healthcare and lost productivity.
      If maternal and child nutrition can be optimised, the benefits will accrue and extend over generations, which is why we must work together now to seize this opportunity.”
End Quote Dr Richard Horton The Lancet
A team led by Prof Robert Black, of Johns Hopkins Bloomberg School of Public Health, Baltimore, US, reviewed evidence on maternal and child under-nutrition and obesity in low-income and middle-income countries since 2008.
      The team also assessed national and international progress on nutrition programmes.
Prof Black and colleagues say while some progress has been made in recent years, they estimate that more than 165 million children were affected by stunting (low height for age) and 50 million by wasting (low weight for height) in 2011.
An estimated 900,000 lives could be saved in 34 countries if 10 proven nutritional interventions were scaled-up to 90% of the world, they say.
"The nutritional consequences of the months during pregnancy and the conditions during the first two years of life have very important consequences for mortality and for adult chronic disease," Prof Black told BBC News.
"The early nutritional deficit results in developmental consequences for the individual and that has implications for their ability to succeed in school and ultimately in society to have the most productive jobs."
The researchers warn that countries will not break out of poverty unless nutrition becomes a global priority.
Dr Richard Horton, editor-in-chief of the Lancet, said: "If maternal and child nutrition can be optimised, the benefits will accrue and extend over generations, which is why we must work together now to seize this opportunity."
Experts working in development are gathering in London this weekend for a summit on nutrition hosted by the UK and Brazilian governments.
This will be followed by the annual summit of leaders from the G8 countries.
The Enough Food for Everyone IF campaign is calling for $1bn per year in additional aid money to be spend on malnutrition by 2015.
Enough Food for Everyone IF spokesperson Anita Tiessen said:
"These new figures confirm our worst fears - that hundreds of thousands more children are dying from malnutrition than we previously thought.

"We have made incredible progress in tackling child deaths around the world, but malnutrition remains the Achilles' heel in our efforts to prevent millions of needless deaths each year. We must urgently prioritise tackling hunger if we are to continue the progress we have made."

R.I.P Albert Mangwea



                                        R.I.P          ALBERT MANGWEA

Wednesday, June 5, 2013

Tanzania to have new constitution in 2014


DAR ES SALAAM - Tanzania will present a new constitution in 2014, a year before its next parliamentary and presidential elections, Prime Minister Mizengo Pinda said on Saturday (25 June 2011), amid opposition pressure for reform.

Pinda said a constitutional review bill is expected to be tabled in parliament by October of this year.

Increasing poverty, unemployment, high food and fuel prices and allegations of corruption have been eroding support for the ruling party in east Africa's second largest economy.

President Jakaya Kikwete was re-elected in an October vote marred by a record low turnout and rigging accusations. He faces an ultimatum from opposition leaders to fix the economy, tackle graft and deliver a new constitution -- or risk mass protests.

Opposition leaders, clerics and rights activists want to limit presidential powers, introduce electoral reforms and allow independent candidates to stand for parliament and president.

Among their demands are a change in the law to allow presidential results to be challenged in court and the formation of an independent electoral commission.

"It is the government's expectations that the new constitution will be complete and ready for inauguration on April 26, 2014, when marking 50 years of the union between Tanganyika and Zanzibar," Pinda said in a statement from the prime minister's office.

Mainland Tanzania (formerly known as Tanganyika) joined with Zanzibar in 1964 to form the Union of Tanzania.

Kikwete has promised to appoint a team to work on a new constitution after growing calls for changes to the country's political system.

Stabilizing Automatic Voltage Regulator



four stage auto-transformer line conditioner with voltage regulation
Automatic voltage stabilizer regulator line conditioner with four-stage auto-transformer, 220V/220vac, 230V/230vac, 600va, 1200va, 1800va.

SLc-E Series
 230V, 600VA, 1200VA and 1800VA
This automatic voltage regulator provides stable power even when the ac mains or back-up generator voltage is extremely low or high. Typical Applications for the SLc E Series
SLc Series conditioners provide low-cost ac line protection for computers, point-of-sale terminals, copiers, data acquisition and control systems, as well as other data processing equipment.
SLc’s can also be used to protect low-cost stand-by UPS to prevent discharge of UPS batteries due to low- or high-voltage transfer to inverter.
Key SLc E Series benefits
TSi Power’s SLc E Series regulated output protects switch-mode power supplies from failure caused by unstable ac mains. SLc provides three-way surge protection and reduction of surge voltage.
The SLc line conditioner can be used between a UPS and the ac mains to provide even greater protection for the connected equipment, while saving the UPS's internal batteries for true black-outs.
How the SLc E Series four stage automatic voltage regulator works
The SLc E Series incorporates a four-winding auto-transformer, which provides four levels of line regulation: two boost-stage and one buck-stage. Even when the input voltage varies between 150 to 280V, the output is regulated to within 200 and 250V, well within the range of most equipment.
SLc E operation is monitored by four status LEDs, indicating normal, boost 1, boost 2 and buck stages of voltage regulation. The front panel power switch turns the SLc E on and supplies power to the equipment.

Key features of the SLc E Series voltage regulator
Four stages of regulated output voltages
Wide input range
Multi-mode surge protection
Quiet operation
Four ac outlets
Front panel power switch
Four status LED display indicators
High efficiency
Low cost
Two year warranty
 Specifications SLc-600E SLc-1200E SLc-1800E
  Electrical

   Capacity in VA (watts) 600VA (600W) 1200 VA (1200W) 1800 VA (1800W)
   Transformer type Four winding auto-transformer
  Input
   Nominal voltage 230 volts ac
   Operating voltage 150 to 280 volts ac
   Nominal frequency  50/60 Hz
   Ac input cord Six foot long ac power cord with IEC-320 plug
  Output
   Ac output voltage 200 to 250 volts ac
   Surge protection Three-way stage surge protection system.
   Surge test conditions Per ANSI/IEEE C62.41-1991 test pulse,
Category A3, Ring Wave, 6000V, 200A
Test pulse injection: Line-neutral, line-ground, and neutral-ground.
   Surge let-through voltages      Remnant Voltage: L-N: 15V, L-G: 15V, N-G: 400V
   Power efficiency > 97% at full load
   Power on/off switch On/off rocker power switch
   Response time Transfers to new stage within 20 cycles of new ac input voltage.
   Transfer time Less than 4 ms between stages.
   Hysteresis 6V minimum. Prevents unnecessary switch-overs
due to momentary ac sags and brownouts.
   Indicators Four status LEDs indicating Normal, Boost 1,
Boost 2, and Buck stages of voltage regulation.
   Ac receptacles Four IEC-320, (E), or two Schuko (with EC Option)
   Audible noise Minimal
  Physical
   Dimensions 152mm(6")wide x 102mm(4")high x 203mm(8")deep
   Weight 3.6 kg (8 lbs) 5 kg (11 lbs) 6.8 kg (15 lbs)
  Safety
   Safety standards Designed to meet UL and IEC standards.
  Environmental
   Ambient temperature 0° to +40°C, 90% relative humidity (non-condensing @ 25.5°C)
  Warranty
   Warranty Two year limited warranty, parts and labor
TSi's ongoing product improvement process makes specifications subject to change. Other companies product names herein are for identification purposes only, and may be trademarks of their respective companies. 
SLc-E Series four tap AVR system architecture  
 Automatic voltage stabilizer regulator line conditioner with four-stage auto-transformer, 220V/220vac, 230V/230vac, 600va, 1200va, 1800va.